Tuesday, July 10, 2012

Mfahamu Mwanamke Mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa Nchini Tanzania....


Tukizungumzia wanawake wajasiriamali wenye mafanikio makubwa nchini Tanzania,huwezi kukosa kumtaja Rita Paulsen ,Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni maarufu ya Benchmark Productions yenye makao yake makuu jijini Dar-es-salaam.

Rita ambaye ana uzoefu wa zaidi ya miaka 12 kwenye masuala ya utengenezaji matangazo na masoko,sio tu ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo yenye mafanikio nchini Tanzania na kimataifa, bali pia ni mmojawapo wa majaji katika show maarufu ijulikanayo kama Bongo Star Search. Show hiyo ambayo hivi karibuni imezidi kujipatia umaarufu mkubwa nchini Tanzania,ni ubunifu mwingine mahiri wa Rita na kampuni yake ya Benchmark Productions.

Rita anasema alianzisha Benchmark kwa sababu kwanza alikuwa anapenda sana kujiajiri na pili wakati ameanza kulikuwa hakuna production house za quality(viwango) vizuri. Aliamini ataweza kubadilisha hilo yaani to make a difference because of  her creativity and the love she has for the work she does.

 
Wanawake oyeeee....!!!!!! Juhudi zako zinaonekana Madam

No comments:

Post a Comment