Wednesday, November 21, 2012

Mjasiriamali anapaswa kujifunza mambo mapya


LEO nitazungumzia  dhana ya ujasiriamali kwamba ni mchakato wa kujifunza.Ujasiriamali hauna mwisho  na ni mchakato wa kujifunza. Hoja hii inathibitishwa na ukweli kwamba mabilionea ulimwenguni walianza hatua ya chini,  wakafanyia kazi mapungufu yao na kuweka mikakati ya mafanikio ya  hapo walipo leo.

Tunaposema ujasiriamali ni mchakato wa kujifunza tuna maana unapofanya biashara kuna mambo mengi unajifunza na kugundua, kuna milima na mabonde umepitia na kufika ulipo leo.

Pamoja na kukutana na vikwazo vya hapa na pale, wajasiriamali bado wana ari ya kuendelea mbele ili wanikiwe zaidi na zaidi. Kitalaam, mchakato wa kujifunza katika ujasiriamali unahusisha namna na uwezo wa kuona fursa ambazo wengine hawazioni na kubadilisha mfumo wa kufanya biashara kizamani na kuwa wa kisasa ambao unazingatia taratibu na maadili ya biashara husika.

Kubadilisha mfumo wa kufanya biashara na kugundua fursa za biashara, yote hayo hayaji kirahisi bali yanatokana na  juhudi binafsi za kutafuta habari na taarifa kupitia vyanzo tofauti.

Moja ya njia za kupata taarifa ni kupata mafunzo, kujisomea vitabu na maandiko mbalimbali kuhusu biashara husika.

Pia mjasiriamani anaweza kupata taarifa kwa njia ya kusafiri na kuona wengine wanafanya nini na kuzungumza na  wajasiriamali waliofanikiwa kuliko wewe. Tumeshuhudia mjasirimali anaanza na biashara A na baada ya muda anakua ameshafikia biashara B na zaidi, yaweza kuwa ni mwendelezo wa ukuaji wa ile ile biashara A au ni baishara nyingine kabisa baada ya biashara A kufa.

Kimsingi wakati mwingine tunajifunza kupitia makosa na uzoefu, yawezekana ulikosea mwanzoni unapoanza biashara au ulikuwa na mapungufu kwa mfano, mtaji mdogo, ujuzi hafifu wa biashara husika, lakini baada ya kukaa katika biashara hiyo kwa muda fulani unakuwa na uzoefu unaokupa ujasiri wa kupambanua mambo mbalimbali.

Mpendwa msomaji unapoona biashara haiendi kama unavyotegemea usikate tamaa, na kwa wewe ambaye haujaanza biashara ila una ndoto ya kumiliki biashara usiendelee kusitasita muda utakutupa mkono amua leo na anza kujipanga kuanzisha biashara. Fanya biashara ukitambua kuna mitihani na majaribu mbalimbali. Usikate tamaa ni mwiko, kila wakati hakikisha unapata uelewa mpya kuhusu mambo yote yanayoizunguka biashara yako.

Tunza kumbukumbu za biashara: mali bila daftari hupotea bila taarifa

Kumbukumbu za biashara ni muhimu sana hata ukizingatia msemo wa wahenga kuwa mali bila daftari hupotea bila taarifa. Hivyo biashara bila kumbukumbu ni sawa na bure. Kumbukumbu zina umuhimu na fadia zake ni kama zifuatazo;

Mmiliki kujua faida halisi ya biashara
Faida ya biashara inatokana na mapato baada ya kutoa matumizi, hivyo ni dhahili ili kupata faida halisi mfanyabiashara anapaswa kuweka taarifa zake za mapato na matumizi kwa usahihi na kweli.

Kulipi kodi halali
Kipengele  80 cha sheria ya kodi ya mapato kinatoa nafuu kwa mlipa kodi anayetunza kumbukumbu zake za biashara. Mfanyabiashara asiyekuwa na kumbukumbu za biashara yake anaweza kudaiwa kodi kubwa kuliko stahili yako. Hivyo kumbukumbu za biashara zinasaidia kulipa kodi stahiki na sahihi.

Husaidia kufuatilia mtiririko wa biashara na mapato
Mtiririko wa biashara unahusisha mambo mengi ikiwemo ununuzi wa bidhaa, gharama za biashara, mauzo, wadeni na wadai na hata mali za biashara. Kwa hiyo, kwa mfanyabiashara kuweka kumbukumbu za biashara zitakuwezesha kujua hali na thamani ya mali, madeni na mtaji wa biashara. Hali kadhalika, mtiririko wa fedha. Kwa ujumla utajua thamani ya biashara yako.

Husaidia kuthibitisha au kutoa ushuhuda wa miamala ya biashara
Mwendelezo wa utunzaji kumbukumbu za biashara hufikia hatua ya kufanya ukaguzi wa mahesabu ambapo wakaguzi wa mahesabu hukagua taarifa hizo ili kutoa ripoti ya taarifa za fedha. Nyaraka zilizotunzwa vizuri mfano, stakabadhi, vocha za malipo na risiti zake ndizo zitathibitisha kuwa kweli muamala ulifanyika na malipo au maingizo ni sahihi.
Mamlaka ya Kodi nchini – TRA na hata benki huhitaji kuona nyaraka hizo hizo za biashara ili kujiridhisha wakati wa kukadiria kodi ya biashara yako hiyo.

Mahitaji ya wawekezaji
Wakati mwingine unaweza kuhitaji kuongeza nguvu/mtaji wa biashara kwa kupitia njia ya kutafuta mwekezaji au mbia, hivyo kumbukumbu ulizonazo ndizo zitakazomfanya mwekezaji au mbia kutoa maamuzi. Na wakati mwingine unaweza kutaka kuuza biashara yako, ili kujua bei au thamani ya biashara hiyo kumbukumbu lazima ziwe zimetunzwa vizuri.

Kuongeza mtaji kupitia mikopo
Watu wengi hutumia njia ya mikopo toka benki au taasisi za fedha kuongeza mtaji wa biashara. Kamwe huwezi hata kusogelea taasisi hizo kama huna kumbukumbu za biashara yako. Ili utembee kifua mbele au taasisi za fedha zikufuate zenyewe kukuomba ukope kwao, ni vyema utunze vizuri kumbukumbu za biashara yako.

Aina ya kumbukumbu za biashara
Cash book – hurekodi taarifa zinazohusiana na fedha taslimu au fedha iliyo benki kuingia (kupokea) au kutoka(kulipa)

MFANO WA CHATI YA CASH BOOK
                                     MWEKE                                               MTOE
Tarehe    Maelezo    Taslimu    Benki        Tarehe    Maelezo    Taslimu    Benki
2.4.11    Mauzo    20,000                        2.4.11    Umeme       3,000  
2.4.11    John kulipa deni      7,000            2.4.11    Usafiri       2,000  
2.4.11    Taslimu        20,000                    2.4.11    Kulipa kodi-TRA        1,500
                                                                 2.4.11    Benki    20,000  
  
  Jumla    27,000    20,000                                     Jumla    25,000    1,500
  
Salio fungia      2,000    18,500                  
                              
5.4.11    Salio anzia    2,000    18,500                  

Chati ya Cash Book ina sehemu kuu mbili yaani mweke na mtoe. Mweke ni sehemu ambayo maangizo yote ya fedha taslimu na benki huandikwa. Mtoe ni sehemu ambayo malipo au fedha iliyotoka huandikwa. Hali kadhalika, kama fedha taslimu imepelekwa benki ni lazima pande zote mbili ziandikwe, upande wa mweke na mtoe.

Mwisho wa kila siku lazima ufunge kitabu chako kwa kupata jumla ya taslimu na benki upande wa mweke na jumla ya taslimu na benki upande wa mtoe. Kisha kupata balansi fungia kwa kuchukua jumla ya upande wa mweke kutoa jumla ya upande wa mtoe. Salio fungia huandikwa upande wa mweke. Na mwisho unafungua mstari wa chini ili kurekodi miamala ya siku inayofuata, chukua salio fungia kuwa salio anzia, kisha mtiririko unaendelea(kama hapo juu).

Petty cash – hurekodi matumizi madogo madogo ya fedha taslimu katika uendeshaji wa kila siku wa biashara.
Debit and Credit note – hurekodi taarifa zisizohusu fedha taslimu. Debit note hutumika kuandika taarifa ambazo unategemea kupokea fedha (mali) na Credit note hutumika kuandika taarifa ambazo unategemea kulipa fedha (deni).
VAT Account – kwa biashara za kuuza bidhaa huwa zinakuwa na namba ya usajili ya ongezeko la kodi  - VRN, hivyo lazima uwe na akaunti maalum kwa ajili ya kodi za VAT.

Purchase day book – hurekodi taarifa za manunuzi ya bidhaa au malighafi kila siku.
Sales day book – hurekodi taarifa za mauzo
Production records – hurekodi taarifa za uzalishaji wa kila siku kwa wenye biashara za viwanda.
Bank statement – hii ni taarifa kutoka benki inayoonesha mtiririko wa miamala ya biashara yako kwa fedha zinazotoka au kuingia kwenye akaunti hiyo. Pia hurekodi makato mbalimbali kama gharama za benki. Ni lazima kila biashara kuchukua taarifa hii toka benki walau mara moja kila mwezi.

Mikataba – biashara nyingi huwa zina mikataba mfano pango, kuleta bidhaa au kuuza bidhaa au huduma. Mikataba hii ni muhimu sana kuwa kumbukumbu za biashara.

Rekodi za kompyuta – biashara zingine hutumia mfumo wa komputa hasa kupunguza kazi za makaratasi. Pia ni muhimu kuhakikisha taarifa zinaingizwa vizuri na kutunzwa sehemu mbalimbali (back up).

Inashauriwa ili uwe na kumbukumbu sahihi ni bora kuhakikisha fedha yote inaingia kwenye akaunti ya benki na matumizi yote hutoka kwenye akaunti ya benki. Hii itasaidi kudhibiti matumizi na kuleta nidhamu ya fedha.

Sunday, October 21, 2012

Maonyesho Ya Wajasiriamali Wanawake Dar


Mh. Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bi. Sophia Simba akishangazwa kwa umahiri na uzuri wa kazi za ubunifu za mmoja kati ya wajasiriamali wanawake walioshiriki Jukwaa la Wanawake Wajasiriamali Tanzania- TWENDE, 2011 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es slaam. Pembeni yake kulia ni Mh. Jerry Silaa, meya wa Halmashauri wa wilaya ya ilala, na kushoto ni Musatafa Hassanali, mjasiriamali mbunifu na muasisi wa TWENDE


Washiriki wa TWENDE 2011, wakisalimiana na Waziri wa Viwanda na Biashara Dr. Cyril Chami mara baada ya waziri huyo kuwatembelea katika banda lao na kujionea bidhaa wanazotengeneza

Washiriki wa Jukwaa la Wanawake Wajasiriamali Tanzania- TWENDE, 2011, kutoka mikoa tofauti ya Tanzania na nje ya nchi wakionyesha bidhaa zao katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam

 TWENDE 2012 KUFANYIKA KWA MWAKA WA TATU SASA · SEMINA NA MAONESHO YA TWENDE NI KUANZIA TAREHE 18 HADI 20 YA MWEZI WA KUMI KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM. · WANAWAKE WAJASIRIAMALI KUELIMIKA, KUUZA BIDHAA ZAO NA KUKUZA MTANDAO WA KIBIASHARA KUPITIA JUKWAA LA WANAWAKE WAJASIRIAMALI TANZANIA- TWENDE
 Jukwaa la Wanawake Wajasiriamali Tanzania- TWENDE linatarajia kufanyika kuanzia tarehe 18 – 20 ya mwezi wa kumi 2012 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. TWENDE imekuwa ikifanyika kila mwaka kwa mwaka watatu sasa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2010, lengo likiwa ni kuwaleta pamoja wanawake wajasiriamali wadogo, wakubwa na wale wanaochipukia ili kupata fursa ya kuuza, kuonesha na kujadili masuala ya biashara kwa ujumla. Sambamba na hilo. TWENDE inalenga kusaidiana na serikali katika kutimiza malengo ya milenia likiwemo lengo namba moja ambalo linalenga kuondoa umasikini, namba tatu kutetea haki na fursa sawa kwa wanawake, lengo namba tano kuhamasisha afya ya uzazi na lengo namba nane, ambayo ni kuendeleza uhusiano wa kudumu kwa ajili ya maendeleo ya jamii. Pia TWENDE inalenga Kukuza uzalishaji kwa wanawake wafanyabiashara na kukuza mgawanyiko wa masoko sambamba na muonekano wa wafanyabiashara wanawake katika jamii. Kwa upande wa mwaka huu TWENDE inatarajia kuwashirikisha wanawake wajasiriamali wengi zaidi ambao wamekuwa wakifanya biashasha tofauti ili kuweza kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kuongeza ujuzi zaidi kibiashara. Sambamba na semina bora zitakazotolewa kwa wanawake wote ambao watapata elimu itakayotolewa wataalamu wa fani mbalimbali Kwa miaka mitatu mfululizo TWENDE imekuwa ikitoa fursa kwa wanawake wajasiriamali kukutana pamoja na kujadili mafanikio na changamoto ambazo zimekuwa ni kikwazo cha wanawake wajasiriamali kutofikia malengo yao kibiashara. “Licha ya kwamba wanawake wengi wamejikita katika sekta hii ya ujasiriamali, lakini bado wamekuwa wakikabiliawa na changamoto mbalimbali zinazokwamisha kufikia malengo yao, ikiwemo elimu ya ujasiriamli na upatikanaji wa mikopo, kwa hiyo ipo haja kwa wanawake kujijengea utaratibu wa kushiriki katika fursa kama hizi zinazowajengea uwezo”. Alisema Saphia Ngalapi Meneja Mradi wa TWENDE. Zaidi ya Wanawake Wajasiriamali Wanawake 100 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani wanatarajai kushiriki katika TWENDE mwaka huu, ampabo maonesho hayo yanakwenda sambamba na semina zitakazo tolewa kwa wanawake wote bure, kwa wale watakaoshiriki katika maonesho, na hata wale ambo watakuwa hawakupata frusa ya kuonesha na kuuza bidhaa zao. KUHUSU TWENDE Tanzania Women Entrepreneurs & Networking Development Exposition (TWENDE) inapanga kuleta maendeleo kwa wanawake wajasiriamali kwa kuandaa jukwaa ambalo litakua mahususi kuweza kukutana zaidi ya wanawake wafanyabiashara 100 wadogo, wakati na wakubwa kutoka viwanda vikubwa na vidogo, taasisi za serikali na mashirika yasio ya kiserikali (NGO). Tanzania Women Entrepreneurs & Networking Development Exposition (TWENDE) pia inalenga kuyapa fursa makampuni kukutana yakikidhi malengo ya wahudhuriaji. Ni sehemu ya kuuza na kuonyesha bidhaa na huduma za kampuni mbalimbali kwa wafanya maamuzi. Maonyesho haya yataenda sambamba na mkutano wa siku tatu utakaotoa elimu bora kwa washiriki. MTAZAMO WA TWENDE Ni kuwaelimisha kuwahamasisha na kuwaendeleza wanawake Tanzania.

MWAMVITA MAKAMBA AHIMIZA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KUTUMIA VEMA FURSA


Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,akiongea na wakina mama wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara, mara alipofika kijijini hapo kutoa mikopo ya kifedha kwa vikundi mbalimbali vya kinamama,ambapo urudishwa kwa njia ya m-pesa bila riba,Mikopo hiyo huendeshwa na Mfuko wa kampuni hiyo MWEI kupitia Vodacom Foundation,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)


Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,akimkabidhi mmoja wa kinamama wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara,fedha za  mkopo  unaolenga kuwakomboa wakinamama hapa nchini, Huduma hiyo hutolewa na Vodacom Foundation kupitia mradi wake wa (MWEI) na kurudisha fedha hizo bila riba kwa njia ya m-pesa,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)


Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,akimshuhudia Glory Muro, wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara,akisaini nyaraka za kupewa mkopo wa kifedha  inayolenga kuwakomboa wakinamama hapa nchini, Huduma hiyo hutolewa na Vodacom Foundation kupitia mradi wake wa kusaidia kinama wa (MWEI) na kurudisha fedha hizo bila riba kwa njia ya m-pesa,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)kulia ni Afisa wa Mradi huyo….


Bi.Johari Mwaselela wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara,akisaini nyaraka za kupewa mkopo wakati  Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,wapili toka kulia alipofika  kijijini hapo kutoa mikopo ya kifedha kwa vikundi mbalimbali vya kinamama,Huduma hiyo ya Mikopo hutolewa na Vodacom Foundation kupitia mradi wake wa kusaidia wakinama MWEI na kurudishwa kwa njia ya m-pesa bila riba,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)kulia ni Afisa wa Mradi huyo Ally Mbuyu,na kushoto ni Meneja wa Mradi huo Mwamvua Mlangwa.


Baadhi ya kinamama wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara, wakiwa kwenye picha ya pamoja na Ofisa Mkuu na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,wanne toka kushoto na Meneja wa Mradi wa MWEI Mwamvua Mlangwa mara baada ya kufika hapo kutoa mikopo ya kifedha kwa vikundi mbalimbali vya kinamama kijijini hapo,Mikopo hiyo urudishwa bila riba kwa njia ya m-pesa,Huduma hiyo hutolewa na Vodacom Foundation kwa kupitia Mradi wao wa  MWEI,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)

Baadhi ya kinamama wa Kijiji cha Mererani Wilaya ya Simanjiro Mkoani  Manyara, wakifurahia jambo wakati walipokuwa wakiongea na Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba,(hayupo pichani) mara alipofika kijijini hapo kutoa mikopo ya kifedha kwa vikundi mbalimbali vya kinamama,Mikopo hiyo urudishwa kwa njia ya m-pesa bila riba,Huduma hiyo hutolewa na Vodacom Foundation kupitia Mradi wa MWEI,zaidi ya kinamama 108 walifaidika na Mkopo huo wa kiasi cha Shilingi Milioni tisa na laki saba,(9,700,000)
---
·         Akabidhi mikopo nafuu kwa vikundi tisa vya Mirerani
·         Ni kupitia mradi wa MWEI

Na Mwandishi wetu.
Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Bi. Mwamvita Makamba amewataka wanawake wajasiriamali hususan wadogo kutambua kuwa maendeleo ya biashara zao na hatimae hali zao za kiuchumi kutategemea pamoja na mambo mengine namna wanavyotumia vizuri fursa za uwezeshaji wanazotengenezewa.

Bi. Mwamvita ametoa changamoto hiyo Wilayani Simanajiro, Mkoani Manyara katika kijiji Cha Mirerani wakati akikabidhi mikopo isiyo na riba wala dhamana yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni Tisa kwa vikundi tisa vya akina mama iliyotolewas na mradi wa Vodacom wa kusaidia wajasiriamali wadogo wanawake wa MWEI.

Bi. Mwamvita amesema kadiri ambavyo wanawake watakuwa tayari kutumia vema fursa wanazotengenezewa ikiwemo ya MWEI wanajiweka katika nafasi nzuri ya kujiwezesha kiuchumi na kuondokana na dhana kwamba mwanamke ni kiumbe tegemezi.
“Wanawake wenzangu leo Vodacom inapowakabidhi mikopo isiyo na riba wala dhamana ni fursa adhimu sana kwenu, ni wajibu wenu kutumia vema fursa hii kujiinua kama ilivyokuwa wajibu wa Vodacom kuwatafuta, kuwafikia na kuwawezesha, kazi sasa ni kwenu”Alisema Bi. Mwamvita.

Bi. Mwamvita amesema kumekuwepo na kilio kikubwa cha wanawake wajasiriamali wadogo kutofikiwa kwa urahisi ama kukosa uwezo wa kukopesheka kutoka taasisi za fedha, hivyo katika kutimiza azma ya kubadili maisha ya watanzania Vodacom ilibuni mradi wa MWEI kutatua changamoto hiyo.

“Ni vigumu kupata taasisi itakayokukopesha mfnyabishara wa vitumbua, genge mchuuzi wa samaki, msusi n.k tena bila riba wala dhamana na zaidi kukupatia mafunzo ya ujasiriamali kwa gharama zake, Vodacom licha ya kwamba biashara yetu ni huduma za simu imethubutu kubuni mradi wa mikopo kwa kuwa inapenda kuona maisha ya watanzania wakiwemo akina mama yanabadilika”Aliongeza Mwamvita

Aidha Bi. Mwamvita amewataka wanawake hao kuhakikisha mikopo waliyoichukua inleta tija katika biashara zao hasa kuinua mitaji ili nao waweze kusimama na kusaidia wanawake wengine.

“Kabla ya kuwakibidhi mikopo hii tumewapatia mafunzo ya ujasiriamali ikiwemo somo la utunzaji wa mahesabu ya biashara, tutumie elimu hiyo na mikopo hii kujiimarisha ili kuinua sauti zetu kwenye jamii”Aliongeza Mwamvita huku akisindikizwa na vigelegele vya furaha kutoka kwa akina mama. 

Mradi wa MWEI ni mahsusi kwa ajili ya kusaidia akina mama nchini kama mchango wa Vodacom kuunga mkono juhudi za kitaifa za kumwezesha kiuchumi mwanamke wa kitanzania na unalenga hasa wanawake wenye biashara zenye mitaji ya  kati ya Sh. 5000 na 200,000
Bi. Mwamvita amesema kuwa mradi wa MWEI umejiwekea lengo la kuwafikia wanawake wengi zaidi hususan maeneo ya vijijini ambao pamoja na kujituma katika bishara ndogondogo wanakabiliw ana uchache wa fursa za uwezeshaji.

“Ni hatua muhimu katika maisha yetu kama Vodacom kusaidia ujenzi wa ustawi wa jamii hapa nchini, tuna namna nyingi ya kubadili maisha ya watanzania kama  dira yetu invyosema, MWEI ni namna mojawapo”. Alisema Mwamvita.

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa mikopo hiyo mbali na kuishukuru Vodacom, wanufaika hao wameahidi kuitumia vizuri mikopo hiyo ili kutimiza malengo ya kibiashara waliyonayo.

“Wengi wetu hapa ni wajasiriamali wadogo tunaojishughulisha na biashara za ususi, mama lishe n.k changamoto kubwa tuliyokuwa tukikabiliana nayo ni kuweza kufikiwa na mikopo nafuu, leo tunafuraha kuona tumepata mikopo isiyo na riba hata shilingi moja” Alisema Johari Mwaselela Mmoja wa viongozi wa Vikundi.

Amesema kupitia vikundi vyao, watahakikisha wanafanya kazi kwa pamoja na kuhimizana ili mikopo waliyopatiwa itoe tija ya kuinua mitaji yao, wakuze faida sambamba na kusaidia kubadili hali zao za maisha.

Tunawaomba Vodacom kama mlivyotufikia sisi hapa kijijini muwafikie na wenzetu wengine waliopo vijijini kama sisi na muwaokoe, kwa kweli wanawke bado tupo nyuma, tunawashukuru sana MWEI.”Aliongeza Mamam Mwaselela.

Awali Meneja wa Mradi wa MWEI Bi Mwamvua Mlangwa alisema hadi kufikia Januari mwaka huu kiasi cha Shilingi 150 Milioni kimeshatolewa na kunufaisha akina mama zaidi ya 6,000
Bi. Mwamvua amesema idadi ya wanaohitaji mikopo hiyo ni kubwa hivyo amewasihi kina mama hao wa Mirerani kutumia vizuri fursa hiyo na kuhakikisha wanarudisha mikopo kwa wakati ili kuwafikia wanawake wa sehemu nyengine nchini.
Kupitia mradi wa MWEI Vodacom huvipatia vikundi vya akina mama mikopo  pamoja na mafunzo ya ujasiriamali kazi ambayo hufanywa na Shirika la kuhudumia viwanda Vidogo – SIDO kwa gharama za Vodacom.

Mikoa ya Arusha, Manyara, Morogoro, Tanga, Rukwa na Katavi, Dodoma, Mara, Mwanza,Shinyanga na Pwani imeshanufaika na mikopo ya MWEI tangu mradi huo ulipoanzishwa mwaka 2011.



Tuesday, August 21, 2012

Juhudi za wanawake wajasiriamali zanzibar......



Beneficiaries of the Women Empowerment in Zanzibar (Weza) project have engaged in clove-soap making to fight abject poverty and boost their incomes.

According to a press statement issued in Dar es Salaam on Sunday by the Tanzania Media Women Association (Tamwa), Weza members in Nganani and Kizimkazi Mkunguni in Unguja South and Piki in Pemba North initiated the project after realising that it was viable and a good deal for making money quickly.

Secretary of one of the beneficiary groups known, as Tupendane, Mahabuba Thabit, from Kizimkazi Mkunguni in Unguja South region, said the soap making initiative was launched mid last year after the members had attended handcraft trainings organised by Weza.
She said the project’s working capital of 199,000/- was spent on soap ingredients such as clove oil, powder, caustic soda and soap cutting equipment.

Mahabuba said in an exclusive interview that the group had manufactured soap two times between June and December, last year during which they earned a profit of 370,000/- in total.

She further said the lack of enough modern cutting machines and packaging facilities remained the main challenge that needs immediate attention, if the project is to flourish sustainably.
Mahabuba called for support from development partners and the government in order to develop the local soap industry and create more jobs, especially for women.

Weza Capacity Building Officer charged with savings and loans, Hakum Sanani, said should soap-making production improve; women in Zanzibar would secure a big market share in the soap-making industry and overwhelmingly improved their livelihood.

The Weza project was initiated three years ago for the purpose of improving the social economic status of rural poor women in Zanzibar, said the Tamwa press statement.

The soaps are available at EmC's Choice Sinza Mapambano 0654450200

Saturday, July 28, 2012

NAMNA YA KUANZISHA BIASHARA.....

Ukitaka kufanya biashara yoyote ile unatakiwa kufanya utafiti. Kutokufanya utafiti ni chanzo cha biashara nyingi kuharibika. Lazima ujiulize kwamba unataka kufanya biashara gani? Usiseme unataka kufanya biashara yoyote ile kwani kusema kwamba unataka kufanya biashara yoyote ile ni kupoteza mwelekeo kwa kuwa utakuwa hujui unataka kufanya nini. Kama hujui cha kufanya hakuna kitu utakachokifanya. Hili ni tatizo la watu wengi. Hata baadhi ya watu niliokutana nao wakitaka ushauri wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo hili. Njia ya kukusaidia kuamua ufanye biashara gani ni kwa kujiuliza umewahi kufanya kazi au biashara gani? Umesomea nini? Vipaji vyako ni vipi? Ni biashara ipi au kazi ipi unapenda zaidi kuliko nyingine na kwa sababu gani? Ukisha jiuliza maswali haya chukua kalamu na karatasi uandike maswali yako na kuyajibu. Ukikagua maswali na majibu yako utagundua shughuli unayoipenda, unayoiweza na una kipaji nayo na hiyo ndiyo inayokufaa. Ukishachagua biashara unayoipenda ni rahisi sana kufanikiwa kwani shughuli utazifanya kwa hiyari bila kujilazimisha. Kama unashindwa kuamua ni biashara gani ufanye, soma sura ya sita katika kitabu hiki. Nimeelezea kuhusu mawazo yanayoweza kukusaidia kuanzisha biashara mbalimbali ambazo unaweza kuzifanya. Kama utakuwa bado hujafikia uamuzi baada ya hapo basi tafuta na wasiliana na washauri ili mbadilishane mawazo na ufundishwe jinsi ya kuamua ufanye biashara gani.
Mambo mengine unayotakiwa kuyafanyia utafiti ni:-
(i) Kujua siri ya bishara unayotaka kufanya ili upate mbinu za kupata mafanikio. Unaweza kupata siri au kujifunza mbinu kutoka kwa watu wanaofanya biashara kama unayotaka kufanya. Suala hili ni gumu sana kwani wafanyabiashara wengi huwa wanaficha siri za biashara zao ili kulinda wasizidiwe maarifa na washindani wao. Unaweza kuipata siri hiyo kama utakwenda kupata ushauri toka kwa mfanyabiashara ambaye yuko mbali na mahali unapofanyia biashara, au tafuta ushauri kwa wataalamu wa mambo ya biashara.
(ii) Fanya utafiti wa soko la bidhaa unazouza au unazotarajia kuuza. Jiulize, je bidhaa unazotaka kuziuza zina soko? Utawauzia watu gani na utauzaje? Kama wewe ni mzalishaji, una mazao / bidhaa unapaswa kuuza kwa jumla, mchanganyiko ama rejareja? Je utatangaza vipi bidhaa zako? Maelezo ya namna ya kutangaza bidhaa zako utayapata katika Sehemu ya Tatu ya Kitabu hiki. Utafiti wa soko unaweza kuufanya kwa kuwauliza wafanya biashara waliotangulia maswali hayo ya utafiti kwani wao wamekuwapo kwenye soko na wanazijua siri za soko.
(iii) Tengeneza bajeti yako kwa kuorodhesha vitu vinavyohitajika na gharama zake ili kuweza kuanzisha biashara yako. Vitu hivyo ni:-
(a) Gharama za Kujenga au kupanga ofisi
(b) Gharama za Leseni ya biashara
(c) Makadirio ya kodi toka TRA
(d) Garama ya vifaa vya ofisi yaani, Samani, makaratasi, mitambo, mashine, nk
(e) Manunuzi ya malighafi au bidhaa za kuanzia biashara
(f) Idadi ya wafanyakazi na gharama za mishahara yao.
(g) Gharama nyinginezo kama vile, umeme, maji, nk.
(iv) Unatakiwa kujua ni mtaji kiasi gani unahitajika kuanzisha biashara yako. Mtaji huo utaujua baada ya kujumlisha gharama zilizoorodheshwa katika kupengele namba (iii)Gharama hizi ni za mwaka ule wa kwanza wa kuanzia
(v) Tafuta Mtaji.
Mtaji unaweza kupatikana kutoka kwenye vyanzo vifuatavyo:-
(a) Akiba au mshahara
(b) Msaada au mkopo kutoka kwa ndugu na jamaa.
(c) Kuingia ubia na mtu mwenye mtaji
(d) Mkopo toka baadhi ya asasi kama vyama vya akiba na mikopo (SACCOS), NGO za kifedha sipokuwa Benki kwani hizi huwa hazitoi mikopo kwa mtu anayeanzisha biashara.

TARATIBU ZA KISHERIA ZA KUFUATA ILI KUANZISHA BIASHARA

Baada ya kufanya utafiti na kupanga mipango ya kuanzisha biashara unatakiwa kwanza kuangalia taratibu za kisheria ambazo unatakiwa kuzifuata na kuzitekeleza. Kama biashara yako ni ndogo anza kama mtu binafsi. Faida ya kuanza biashara kama mtu binafsi ni urahisi wa kuanzisha biashara; urahisi na wepesi wa kutoa maamuzi kwani huhitaji ridhaa ya mtu mwingine kabla ya kutoa uamuzi; mtaji unaohitajika utakuwa mdogo kutokana na gharama za uendeshaji kuwa ndogo, biashara hii inaweza kuendeshwa kwa msaada wa familia kwa kumtumia mke au mume, watoto au ndugu na jamaa na raslimali za familia kama nyumba na samani. Unapoanzisha biashara na kuiendesha mwenyewe unakuwa huru tofauti na mifumo mingine. Matatizo ya kufanya biashara kama mtu binafsi ni:- Kushindwa kupanua biashara yako kwa ufinyu wa mtaji; kufilisiwa mali zako za binafsi iwapo biashara yako itafilisika kwani katika mfumo huu mali ya biashara na mali binafsi si rahisi kuzitenganisha; Kuongeza mtaji inakuwa ni vigumu, hivyo unaweza kushindwa kupanua biashara yako. Ili kuepukana na matatizo niliyoyataja hapo juu unaweza kuungana na watu wengine kufanya biashara kwa ubia. Faida za kufanya biashara kwa ubia ni: Kupata fursa ya kuongeza mtaji kwa kushirikiana na wafanyabiashara wengine ambao wataleta mitaji yao; Kuongeza ujuzi katika shughuli kwa kuleta wataalamu pale taaluma Fulani inapohitajika. Matatizo ya kuendesha biashara kwa njia ya ubia ni: Kufilisiwa mali zako binafsi endapo biashara yako itafilisika; kudhulumiana mali endapo moja wa wabia atakuwa si mwaminifu ambapo anaweza kuingia mikataba mibovu na kusababisha hasara ambayo itabebwa na wabia wote. Ni muhimu kuwachunguza watu tunaotaka kujiunga nao ili tujue kama ni waaminifu. Pia ni vyema kuwapo na mkataba wa maandishi mnapoanzisha biashara ya ubia mkimshirikisha mwanasheria kama shahidi ili kujikinga na kudhulumiana; Kufariki kwa mbia mmoja kunaweza kusababisha kuvunjika kwa ubia; kotokuelewana kwa wabia kunaweza kusababisha kuvunjika kwa ubia. Kama biashara ikikua unaweza kuanzisha kampuni. Mfumo wa uendeshaji wa kampuni unazo faida zifuatazo: unatenganisha majukumu ya wamiliki mali na kampuni yaani kampuni inaposajiliwa inakuwa inakuwa na hadhi na kutambulika kisheria kama ni mfumo tofauti na wamiliki. Mfumo huu unatenganisha majukumu kati ya menejimenti na wamiliki wa kampuni; madeni ya kampuni yatalipwa hadi kufikia kikomo cha mtaji uliowekezwa na wamiliki. Hivyo, mali binafsi za wamiliki wa kampuni haziwezi kukamatwa kufidia madeni ya kampuni endapo kampuni itafilisika. Mfumo wa kampuni unatoa nafasi ya kupanua mtaji kwa kukusanya mitaji kwa kuongeza wanahisa au kupitia soko la mitaji ya hisa. Mfumo huu ndiyo unafaa kwa biashara kubwa kwani unatoa nafasi ya kupanuka kwa biashara na kuendelea kuwapo kwa biashara hata kama baadhi ya wamiliki wake wakifa au kujitoa katika kampuni.

Mambo ya muhimu ya kutekeleza kisheria kabla ya kuanzisha biashara ni:-


(a) Kuwa na ofisi
(b) Kukata leseni
(c) Kusajiliwa na TRA kama mlipokodi na kupewa namba ya mlipakodi
(d) Kufanyiwa makadirio ya kodi ya mapato ya awali
(e) Kutimiza masharti mengine ya keshiria kuwa mfano kama wewe unataka kufanya biashara ya ukandarasi wa ujenzi wa majengo lazima usajiliwe kwenye Bodi ya Wakandarasi.

Kama unafanya biashara ya kati au kubwa unapaswa kufuata sheria. Ni makosa kufanya biashara bila kufuata sheria za nchi. Hata hivyo, kuna biashara zingine ndogo ndogo sana kiasi kwamba uanzishaji wake si rahisi kufuata sheria hizo hapo juu, mfano uuzaji wa maandazi, karanga na vitu vingine vidogovidogo. Hizi zinaitwa biashara zisizo rasmi au biashara ndogondogo. Ni vyema ukachunguza kama biashara unayoifanya ni ndogo au kubwa ili ujue kama unapaswa kufuata taratibu za kisheria au la, kwani kutokujua utaratibu na sheria siyo kinga ya kukufanya usishitakiwe.



Tuesday, July 10, 2012

UJASIRIAMALI---UFUGAJI BORA WA KUKU WA KIENYEJI


Idadi ya wanyama wanaofugwa kwa chakula imezidi ile ya binadamu zaidi ya mara mbili kote ulimwenguni. Kuna maelfu ya wanyama kote duniani ilihali ni wachache tu wanaoweza kufugwa. Kati ya hawa wanyama, ni aina nne (Ng'ombe, kondoo, mbuzi na kuku) wanaochukua asilimia 95% ya wanyama wote wanaofugwa. Wanyama hawa hupatikana katika nchi za hari kwenye nyanda za chini. Lakini kati ya mifugo hawa, kuku ni maarufu katika nchi za hari na hata kote ulimwenguni.

Lengo la makala haya ni kutoa maelezo ili kusaidia wafugaji wa kiwango kidogo katika nchi
zinazostawi, katika kupunguza umaskini. Sehemu ya kwanza (I) itatoa maelezo kuhusu ufugaji na hasa ufugaji wa kuku, Sehemu ya pili (II) itaangazia maswala yafuatayo katika kuinua hali ya uchumi kwa kufuga kuku:

1. Kuendeleza ufugaji wa kuku za kienyeji kwa kutumia njia zisizohitaji gharama nyingi.
2. Kutafuta mbinu na njia muafaka za kuzalisha viwango vya kuku bora kwa njia ya kiasili.
3. Matumizi ya njia za kiasili au zile zisizo gharimu pesa nyingi kutibu na kuzuia magonjwa ya kuku.

SEHEMU YA I: MAELEZO KUHUSU UFUGAJI WA KUKU KATIKA NCHI ZINAZOENDELEA

NAFASI YA MIFUGO
Licha ya kukosa mashamba makubwa ya kuendeleza ufugaji wa ng'ombe, jamii nyingi katika nchi za hari (tropics) hupata nafasi ya kufuga kuku kwa kiwango kidogo.

Idadi ya wanyama wanaofugwa huongezeka sambamba na ile ya watu. Idadi ya watu inapoongezeka ndipo ile ya mifugo huzidi.

Idadi kubwa ya watu huhitaji chakula kingi na matumizi huongezeka, hivyo basi watu hufanya bidii kuzalisha chakula na mapato kutoka kwa shamba.

Ufugaji wa ng'ombe na wanyama wanaohitaji lishe kwa wingi huhitaji kiasi kikubwa cha shamba ili kupanda mimea na lishe la mifugo. Ukilinganisha na ufugaji wa kuku, utahitaji mabaki ya vyakula na sehemu ndogo ya shamba. Ufugaji wa kuku umeweza kunawiri hata pasipo fedha.

Katika nchi za hari ufugaji wa kienyeji hautahitaji kazi nyingi, kazi hii hufanywa na akina mama na watoto. Kwa kawaida katika nchi hizi kazi nyingi za nyumbani hutekelezwa na mama. Vyakula vya kuku vyaweza kutoka kwa: 1) Mabaki ya chakula, 2) Mabaki ya mimea, 3) Mabaki kutoka jikoni na 4) Vyakula vya kujitafutia (kwa mfano kwekwe, mbegu, wadudu, nyongonyongo, n.k).

Mfumo wa kufuga kuku kwa njia ya kienyeji hutumia viungo vinavyopatikana kwa urahisi na kuimarisha hali ya kiuchumi na chakula bora kwa jamii.

Ni muhimu sana kufuga mifugo hata ikiwa ni kwa kiwango kidogo kwa sababu ya 1) Chakula bora na kuongeza mapato ya jamii kwa viwango vya kuridhisha; 2) Mifugo ni hakiba au banki, faida yakehuzaana tu kama riba ya benki; 3) Mifugo yaweza kuuzwa ili kugharamia karo ya wanafunzi,malipo ya hospitali, gharama nyingine za nyumbani na hata shambani; 4) Kwa matumizi ya kijamii (kwa mfano kulipia mahari, shughuli za kidini, n.k); 5) Mifugo husaidia katika kukabili wadudu,kwekwe na kuimarisha rutuba kutokana na mbolea ya kinyesi. Ni bayana kwamba mifugo ni muhimu sana kwa mkulima yeyote yule.

UMUHIMU WA UFUGAJI WA NJIA YA KIENYEJI
Ufugaji wa kuku katika nchi zinazostawi waweza kugawanywa mara mbili: 1) Ufugaji wa
kitamaduni au kienyeji pasipo kuwepo gharama, na 2) Ufugaji wa kisasa unaohitaji fedha nyingi.

Ufugaji wa viwango vikubwa kwa kuzingatia mfumo wa kisasa ni maarufu katika kuzalisha kuku wa nyama na wale wa mayai. Mfumo huu hujumuisha asilimia ndogo sana ya aina ya ufugaji.

Itafahamika kwamba mfumo wa kisasa haujaadhiri ule wa kienyeji. Idadi kubwa ya watu katika nchi za hari hutegemea mfumo wa kienyeji kwa nyama na mayai.

Mfumo wa kisasa huhitaji pesa nyingi za kununua vyakula vya kuku. Aidha mfumo wa kisasa huhitaji kazi nyingi ili kutekeleza. Mfumo wa kisasa umefaulu katika nchi zilizostawi kutokana na hali nzuri ya kiuchumi katika kuzalisha (kuku wa hali ya juu, kuangua vifaranga kwa stima, vyakula vilivyo na madini mengi, vifaa na zana za mashine,utaalamu wa hali ya juu n.k). Haitafaa sana kuanzisha mfumo kama huu katika vijiji vya mataifa yanayostawi.

"Mageuzi" katika ufugaji (kuambatanisha mfumo wa kisasa pamoja na ule wa kienyeji) yamefanyiwa majaribio katika mataifa yanayostawi tangu miaka ya 1950.

Matokeo ya kuku wapatao 200 hadi 300kwa shamba moja hayajawai kufaulu. Hasara imepatikana na waweza kuona nyumba zilizokuwa na kuku bila chochote, pesa nyingi zimepotea na kuku hawapo.

Mfumo wa kienyeji ni bora (Katika hali ya kiuchumi) iwapo idadi ya kuku haitazidi kuku 50. Ni rahisi kuweza kuwatunza kuku, kwani hakuna gharama nyingi. Iwapo vyakula au zana za kisasa zitanunuliwa, basi haitakuwa kwa viwango vikubwa. Mazao ya nyama na mayai yataleta faida.

Sehemu nyingi katika mataifa yanayostawi hakuna stima, katika nchi za hari, ufugaji kwa kiwangokidogo umeweza kufaulu na kuimarisha uchumi.

FAIDA ZA UFUGAJI WA KUKU KWA NJIA YA KIENYEJI
Faida za uzalishaji kuku ili kuimarisha uchumi kwa njia hii zimepuuzwa na viongozi na wafadhili.

Kuku huleta faida kwa jamii kama tulivyoona katika sehemu ya I. Zaidi ya hayo, ufugaji wa kuku waweza kuimarishwa pasipo gharama nyingi ukilinganisha na mifugo wengine.
· Hutupatia fedha kwa kuuza nyama na mayai
· Mayai ni chakula kilicho na madini muhimu na kisicho ghali katika soko lolote. (madini kama methionine na cystine), madini haya ni muhimu sana kwa afya ya watu hasa watoto wachanga. Pia hutupatia protini.
· Kinyesi cha kuku ni mbolea safi
· Kiwanda asilia cha kutotoa vifaranga
· Gharama za kuanzisha na kuendeleza ni nyepesi
· Kitoweo chepesi na rahisi kwa wageni, kitoweo hakihitaji hifadhi hutumika mlo mmoja au miwili na kumalizika
· Jogoo hutumika kama saa inapowika
· Manyoya ya kuku hutumika kutengenezwa mapambo mbalimbali, mito na magodoro
· Kuku wanahisimu wadudu waharibifu

Kuku ndiye mnyama wa kipekee anayeweza kuishi mahali popote hapa ulimwenguni bila kuadhiriwa
na viwango vya hali ya hewa. Ufugaji wa kuku ndio shughuli inayofanyika kwa wingi duniani kuliko ufugaji wa aina yeyote. Kuku hunawiri vyema katika nchi za hari kutokana na uwiano uliopatikana wakati wa mwanzo binadamu alipofuga Asian jungle fowl aina ya kuku-mwitu. Mayai pia yaweza kuhifadhiwa kwa urahisi na huchukua nafasi ndogo kuliko aina ya bidhaa zozote za mifugo. Mayai yaweza kuwekwa mahali kwa muda mrefu bila kuhitaji barafu. Hautahitaji kuhifadhi kuku kwa njia yoyote, kwani nyama yake hupatikana pale unapohitaji kwa kuchinja.
Upungufu wa kuku wa kigeni ukilinganisha na wale wa kienyeji ni kama ufuatao:
• Kuku wa kigeni hawawezi kukalia na kuangua mayai, hivyo basi wahitajika kununua vifaranga (gharama);
• Vifaranga wa kigeni huhitaji utunzaji maalum na vyakula maalum (gharama);
• Kuku waliozalishwa kwa njia ya kisasa huhitaji chakula kingi ili kutaga mayai (gharama);
• Kuku wa kisasa huhitaji zaidi kuchanjwa dhidi ya magonjwa (gharama)ukilinganisha na wa kienyeji (japo nao huhitaji chanjo);
• Kuku wa kutaga mayai huhitaji mwangaza wa stima (saa 14 kwa siku) ili kutaga mayai (gharama)
Kwa kuongezea, rangi ya nyama na mayai ya kuku wa kienyeji huvutia kuliko ile ya kuku wa kisasa.
Hivyo basi jaribu kuendeleza na kuhimiza ufugaji wa kuku wa kienyeji.
Iwapo mkulima ana jogoo mmoja na kuku kumi na mbili, basi kila mwezi waweza kupata kuku akikalia mayai 10-12 kwa mwezi (mayai yote kwa wakati mwingi hayataanguliwa) kuna hakikisho la kupata vifaranga vinne kila mwezi. Kuku mzima atachukua miezi minne kuchunga vifaranga walioanguliwa.

Kwa hivyo, kati ya kuku wote kumi na mbili kila mara kutakuwa na kuku wanne wakitunza vifaranga, huku wale wengine wanane wakitaga mayai.

Kuku waliofugwa kwa njia ya kitamaduni hupata vyakula vyao kwa kutafuta mbegu, wadudu
nyongonyongo, n.k; Lakini kuku hawa hukosa vyakula vya kutosha vilivyo na nguvu ili waweze kutaga mayai. Vyakula vya kutoa nguvu daima huwa ni haba.

Waweza kuwalisha kuku kwa nafaka ili wapate chakula cha nguvu (mfano kilo moja ya nafaka iliyopondwa kila siku kwa kuku 10), nafaka hii yapaswa kuwa kavu. Vifaranga wapewe kiasi kidogo cha nafaka au mchele wiki za kwanza. Kuku wanaolishwa nafaka baada ya kujitafutia chakula nje huongeza idadi ya mayai (kutoka asilimia 20-25% hadi 40-50%). Kuna umuhimu wa kuhifadhi nafaka kama lishe badala ya kuuza kwani utapata mayai mengi ambayo baadaye utaweza kuuza.

Hautahitaji kununua vyakula vya protini kwani kuku hujitafutia lishe la protini.
Ikiwa hauna nafaka, waweza kutumia vyakula vya mzizi au ndizi. Vyakula vya aina hii hata hivyo, huwatatiza kuku wanapovitonogoa, kiwango cha mayai sio kikubwa kama cha wale wanaolishwa nafaka.

Kwa kuwalisha kuku kwa nafaka utapata hakikisho la mayai manne kwa siku kutoka kwa wale kuku wanane. Iwapo hakuna nafaka, kati ya kuku wanane wanaotaga utapata mayai mawili tu kwa siku.

Ni bora kutumia nafaka hii kama lishe kuliko kuuza na hatimaye kununua vyakula vya dukani.

Kuku kumi na mbili na jogoo mmoja wanaolishwa kwa kilo moja ya nafaka kila siku waweza
kuelezwa hivi:
• Waweza kuuza kuku wanne kila mwezi na kujaza pengo hilo na wale vifaranga (vifaranga
wanne huanguliwa kila mwezi) na
• Dazani kumi za mayai kila mwezi (mayai manne kila siku).
Kwa mwaka mmoja waweza kukadiri ile faida utakayopata na vile hali ya kiuchumi yaweza
kuinuliwa katika mataifa yanayostawi.
Hata hivyo faida hii haitaafikiwa iwapo magonjwa
hayatazuiwa au kukabiliwa kama ifuatavyo.

TEKELEZA UTARATIBU WA KUZUIA MAGONJWA

Magonjwa ndio husababisha hasara katika mfumo wa ufugaji wa kuku. Kuku waliochanjwa dhidi ya magonjwa hudumisha afya bora. Jaribu kila mara kuzuia magonjwa, kwani kuzuia ni bora kuliko kuponya. Kinga yaweza kutolewa mara kwa mara (kila baada ya miezi mitatu) dhidi ya magonjwa yafuatayo:

Ugonjwa wa Newcastle
Ugonjwa huu ndio huadhiri kuku na kusababisha hasara katika nchi za hari. Virusi vya ugonjwa huu huenea kwa kasi na rahisi kiasi cha kusababisha vifo kwa asilimia 100%. Dalili za kwanza ni shida ya kupumua na kung'amua hewa, sauti kama ya kikohozi na kutokwa mate. Kinyesi chaweza kuwa na rangi ya kijani kibichi. Hadi sasa hakuna dawa.

Waweza kuzuia ugonjwa huu kwa kutoa chanjo. Dawa za chanjo hupatikana kote ulimwenguni hata katika nchi za hari kwenye vipimo vya vitone mia moja. Madawa haya yaweza kuhifadhiwa kwa muda. Waweza kuweka kwa wiki moja mbali na jua au joto kali (Chanjo hii ni ya kipekee, kwani aina nyingine ya chanjo huwekwa kwa friji). Waweza kutoa chanjo kwa kutia vitone kwenye mdomo. Kuku wote (wakubwa kwa wadogo) wapaswa kupewa chanjo baada ya kila miezi mitatu.

Minyoo
Minyoo kama chango (roundworms) na tegu (tapeworms) huadhiri kuku wa kienyeji. Kuku hukosa hamu ya chakula, mayai hupungua na magonjwa mengine hushambulia. Ni bora basi kutoa minyoo.

Mchanganyiko wa madawa ya aina tatu ndio hutumiwa kuangamiza minyoo, madawa haya ni piperazine, phenothiazine na butynorate. Madawa haya hupatikana kama vidonge (tumia kidonge 1 kwa kuku mzima na 1/2 kwa vifaranga). Iwapo hautapata dawa hii, waweza kutumia Panacur au dawa nyingine ya kuangamiza minyoo. Wapatie kuku dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu.
Wadudu
Wadudu kama chawa au utitiri husumbua kuku katika ufugaji wa kienyeji. Chawa au utitiri
husababisha harara ya ngozi, kuku walio adhiriwa hupata shida na kukosa usingizi. Hali hii
hupunguza kiwango cha mayai na uzito wa kuku.

Tumia asilimia 5% ya unga wa malathion kwa kupulizia kuku (puliza kwa chupa uliyo toboa
mashimo) pulizia kila kuku ili kuzuia chawa na utitiri (kilo moja ya unga huu yaweza kutibu kuku 150). Pulizia dawa hii baada ya kila miezi mitatu, waweza kupuliza kwa wakati mmoja wa kutoa chanjo na dawa zilizotajwa hapo juu. Puliza unga huu pia kwenye viota vya kuangulia mayai.

Waweza kutayarisha 5% ya malathion kwa kuchanganya 25% ya unga wa malathion (kiwango cha kilimo) na sehemu nne za jivu kutoka jikoni.
Magonjwa ya mapafu
Magonjwa ya mapafu huadhiri njia inayopitisha hewa na kuambatanisha mate na sauti kama ya kikohozi. Ugonjwa huu huenea polepole. Uambukizanaji pia hutokea kwa polepole na vifo sio kwa wingi.

Hata hivyo, kutaga mayai na uzito hupungua. Shida hii yaweza kusambaa hata kutoka mahali vifaranga huanguliwa hadi pale walipouzwa.

Tylosin19 ndio dawa inayoweza kutibu magonjwa ya mapafu. Kiasi cha 35mg ya tylosin hutosha kuku mmoja (kiwango hiki hufaa kuku na hata vifaranga) dawa hii husimamisha madhara kutokana na magonjwa ya mapafu.

Tibu kuku kila baada ya miezi mitatu, waweza kutekeleza kwa wakatimmoja wa kutoa kinga na kuangamiza minyoo. Tylosin hupatikana kwa pakiti ndogo ya 4gm.
Waweza kutayarisha dawa hii kwa kutumia maji na 35gm ya tylosin (gramu nne kwa vikombe viwili vya maji), kiasi hiki chaweza kutolewa kwa vitone kwa kila kuku.
KWA UFUPI (SUMMARY)
Kabila za Kuku
Si rahisi kupata kabila halisi (pure breed) au kizazi halisi (pure line) za kuku wa kienyeji kutokana na mwingiliano wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Lakini hata hivyo baadhi ya kuku wa kienyeji wanaweza kutambuliwa kutokana na maumbile yao kwa mfano
1. Kuchi
  • Warefuna wenye kusimama mgongo ukiwa wima
  • Wana manyoya machache mwilini na vilemba vyao ni vidogo
  • Majogoo huwa na wastani wa kilo 2.5 na mitetea kilo 1.8
  • Mayai gram 45
2. Ching'wekwe (Umbo dogo)
  • Hupatikana zaidi Morogoro na umasaini
  • Majogoo kilo 1.6
  • Mitetea kilo 1.2
  • Yai gram 37
  • kuku hawa wanafaa sana kwa biashara ya mayai kwa kuwa hutaga mayai mengi sana.
3. Umbo la Kati
  • Majogoo kilo 1.9
  • Mitetea kilo 1.1
  • Mayai gramu 43
  • Hukua upesi na hupata kinga upesi baada ya kuwachanja dhidi ya ugonjwa wa Mdondo (New Castle)
4. Singamagazi
  • Hupatikana zaidi Tabora
  • Majogoo wana rangi ya moto na mitetea rangi ya nyuki
  • Majogoo kilo 2.9
  • Mitetea kilo 2
  • Mayai gramu 56
5. Mbeya
  • Wanapatikana Ileje Mbeya na asili yao ni Malawi
  • Mjogoo kilo 3
  • Mitetea kilo 2
  • Mayai gramu 49
  • Uwezo wao wa kuatamia mayai na kuangua ni mdogo sana ukilinganisha na kuku wengine
6. Pemba
  • Maumbo ya wastani na miili myembamba
  • majogoo kilo 1.5
  • mitetea kilo 1
  • mayai gramu 42
7. Unguja
  • Hawatofautiani sana na wa Pemba
  • Vilemba vyake ni mchanganyiko- vidogo an vikubwa
  • Majogoo kilo 1.6
  • Mitetea kilo 1.2
  • Mayai gramu 42
SIFA WA KUKU WA KIENYEJI
  1. Wastahimilivu wa Magonjwa
  2. Wana uwezo wa kujitafutia chakula
  3. Huatamia, kutotoa na kulea vifaranga
  4. Wanastahimili mazingira magumu(ukame, baridi n.k)
  5. Nyama yake ina ladha nzuri
KATIKA KUWAENDELEZA KUKU WA KIENYEJI NI VYEMA
  1. Wajengewe nyumba bora
  2. Wapewe kinga dhidi ya ugonjwa wa Mdondo (New Castle), Ndui (Fowl Pox) pamoja na kinga ya minyoo.
  3. Malezi bora ya vifaranga
  4. Kuwapatia chakula cha ziada pamoja na maji ya kunywa ya kutosha.
NYUMBA BORA
Eneo inapojengwa nyumba au banda la kuku liwe
  • Linafikika kwa urahisi
  • Limeinuka juu pasituame maji
  • Pasiwe na pepo zinazovuma
Vifaa kama miti, nyasi, makuti, fito, udongo mabanzi ya miti, cement, mabati n.k
Sifa za Nyumba Bora ya Kuku
  • Paa imara lisilovuja
  • Kuta zisiwe na nyufa
  • Sakafu isiwe na nyufa
  • Madirisha ya kutosha kupitisha hewa
  • Iwe na mlango wa kuingia kufanya usafi
  • Iwe na ukubwa (nafasi) unaolingana na idadi ya kuku. Wastani wa kuku 10-15 kwa mita moja mraba
Mambo muhimu ndani ya nyumba
  • Chaga za kulalia kuku
  • Sakafu iwekwe maranda (wood shavings), makapi ya mpunga, n.k
  • Viota vya kutagia mayai sentimita 35x35x35 na idadi ya viota iwe nusu ya idadi ya kuku waliofikia hatua ya kutaga na viwekwe sehemu iliyojificha (faragha)
UATAMIAJI WA MAYAI
Kuna njia 2
  • Njia ya kubuni (incubators)
  • Asili
Kumuandaa kuku anayeatamia
  • Weka maranda au majani makavu ndani ya kiota
  • Anapokaribia kuatamia toa mayai ndani ya kiota pamoja na maranda, hakikisha mikono haina manukato
  • Nyunyiza dawa ya kuua wadudu (viroboto, utitiri n.k) ndani ya kiota, pia mnyunyizie dawa kuku anayetarajia kulalia mayai
  • Rudisha mayai kwenye kiota ili kuku aanze kuatamia
  • Kwa kawaida kuku hulalia mayai yake kwa muda wa siku 21 ndipo huanguliwa
ULEAJI WA VIFARANGA
Kuna njia mbili
  • Njia ya kubuni
  • Njia ya asili
Njia ya ASILI

Kuku mwenyewe hutembea na vifaranga akivisaidia kutafuta chakula. Ni vizuri kumtenga kuku mwenye vifaranga katika chumba chake pekee ili vifaranga wasishambuliwe na kuku wengine hali kadhalika kuwalinda na wanyama na ndege wanaoshambulia vifaranga.

Njia ya KUBUNI

Vifaranga huwekwa kwa pamoja kwenye chumba maalum na kupatiwa joto maalum, chakula pamoja na maji. Tumia taa ya kandili (chemli), umeme au jiko la mkaa na hiyo taa iweke kwenye mzingo(mduara) walipo vifaranga. Pia kuna kifaa kinaitwa Kinondoni Brooder ni kizuri kwa kutunzia vifaranga. Kwa kutumia kifaa hiki kuku wanaweza kunyang'anywa vifaranga vyao mara tu baada ya kutotoa na kuviweka kwenye hii brooder na hao kuku wakaachwa bila vifaranga vyao, baada ya majuma matatu au manne, kuku hao huanza tena utagaji na kuendelea na uatamiaji hadi kutotoa tena. Kwa mtindo huu kuku anaweza kutotoa mara 5-6 badala ya kama ilivyo sasa mara 2-3 kwa mwaka. Vifaranga vikae ndani ya brooder majuma 3-4 na baadaye fungua milango ya brooder kuruhusu vifaranga vitoke na kuzungukazunguka chumbani bila kuvitoa nje kw kipindi cha mwezi mmoja au zaidi kutegemeana na mazingira.

KULISHA KUKU WA KIENYEJI

Kuku mkubwa huhitaji gramu 120 za chakula kwa siku, ni vizuri kuku wanaofugwa huria (free range) kupatiwa chakula cha ziada gramu 30 kila siku nyakati za jioni.
Kuku walishwe
  • Mizizi-mihogo, viazi vitamu, mbatata, magimbi, n.k
  • Nafaka-mahindi, Mpunga, Mtama, Ulezi na Pumba za nafaka zote
  • Mboga-Mikundekunde, nyanya, milonge, majani ya mapapai
  • Matunda-Mapapai, maembe, n.k
  • Mbegu za Mafuta-Karanga, ufuta, mashudu ya pamba, alizeti, n.k
  • Unga wa dagaa
  • Maji
KUCHANGANYA CHAKULA CHA KUKU
  • Pumba.............kilo20
  • Mashudu ya Pamba n.k...kilo 3
  • Dagaa iliyosagwa.........kilo 1
  • Unga wa majani uliokaushwa kivulini na kusagwa........kilo 2
  • Unga wa Mifupa ..........kilo 0.25
  • Chokaa ya mifugo ........kilo 0.25
  • Chumvi........................gramu 30
  • Vichanganyio/Premix...gramu 25
KUPANDISHA
  • Uwiano wa mitetea na jogoo ni mitetea 10-12 kwa jogoo mmoja
  • Sifa za mtetea ni mkubwa kiumbo, mtagaji mayai mengi, muatamiaji mzuri na mlezi wa vifaranga
  • Sifa za jogoo ni awe mkubwa kiumbo, miguru imara na yenye nguvu, mrefu, upanga/kilemba kikubwa, awe na uwezo wa kuitia chakula mitetea na awe na tabia ya kupenda vifaranga
  • Jogoo huanza kupanda akiwa na umri wa miezi 7-10 na kuendelea hadi miaka mitatu na asipande watoto wake
  • Mitetea huanza kutaga wakiwa na miezi 6-8
MAGONJWA YA KUKU
1. Mdondo/New castle
Virus vinavyosababisha ugonjwa huu huenezwa kwa hewa
Dalili
  • Kuhalisha choo cha kijani na njano
  • Kukohoa na kupumua kwa shida
  • Kupinda shingo kwa nyuma
  • Kuficha kichwa katikati ya miguu
  • Kukosa hamu ya kula na kunywa
  • Idadi kubwa ya vifo hadi 90%
Kinga
  • Chanjo (New Castle vaccine) kwa mpango wa siku 3, wiki 3, miezi 3
  • Epuka kuingiza kuku wageni
  • Choma au fukie mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa
  • Zingatia usafi wa mazingira
NDUIYA KUKU/ FOWL POX
Virus huambukizwa kupitia jeraha au mbu
Dalili
  • Vidonda vyenye utando wa kahawia/purple kwenye sehemu zinazoonekana
  • Kukosa hamu ya kula
  • Vifo vingi
Kinga
  • Chanja vifaranga wanapofikia mwezi 1-2 kwa kutumia chanjo ya Fowl pox vaccine
  • Epuka kuingiza kuku wageni
  • Zingatia usafi wa mazingira
HOMA YA MATUMBO/FOWL TYPHOID
  • Kuharisha kinyesi cha kijani na nyeupe
  • Kuku hukosa hamu ya kula
  • Kuku hukonda
  • Vifo hutokea kidogo kidogo kwa muda mrefu
  • Kinyeshi hushikamana na manyoya
Tiba
Dawa aina ya antibiotic, sulfa na vitamini
Kinga
  • Usafi
  • Fukia mizoga
  • Usiingize kuku wageni
  • Chinja kuku wote mara ugonjwa huu ukiingia na safisha banda, pia pumzika kufuga kwa miezi 6
MAFUA YA KUKU/INFECTIOUS CORYZA
Hutokana na bakitelia na hushambulia hasa kuku wakubwa
Dalili
  • Kuvimba uso
  • Kamasizilizochanganyikana na usaha unaonuka
  • Macho huvimba na kutoa machozi na pengine upofu
  • Hukosa hamu ya kula
  • Mbawa huchafuka na kutoa harufu mbaya
Tiba
Dawa za Antibiotic, sulfa na vitamini
KUHALISHA DAMU/COCCIDIOSIS
Husababishwa na vijidudu vya Protozoa
Dalili
  • Kuharisha damu
  • Manyoya husimama
  • Hulala na kukosa hamu ya kula
MINYOO
Dalili
  • Kunya minyoo
  • Hukosa hamu ya kula
  • Hukonda au kudumaa
  • Wakati mwingine hukohoa
Tiba
Dawa ya minyoo/Pipeazine citrate kila baada ya miezi mitatu
WADUDU
Viroboto, chawa, utitiri
Dalili
  • Kujikuna na kujikung'uta
  • Manyoya kuwa hafifu
  • Rangi ya upanga kuwa hafifu
  • Ngozi kuwa nene, ngumu na yenye magamba yanayodondoka kama unga
Kuzuia
  • Ziba mipasuko sakafuni na kwenye kuta za banda
  • Fagia banda mara mbili kwa wiki
  • Nyunyiza majivu au chokaa mara moja kwa wiki mara baada ya kufagia
  • Choma masalia ya mayai yaliyoanguliwa
  • Nyunyiza dawa kwenye viota
  • Weka maranda, majani makavu, makapi ya mpunga ya kutosha sakafuni ndani ya banda la kuku
  • Fuata kanuni za chanjo
  • Tenga kuku wagonjwa wakae mbali na kuku wazima
UPUNGUFU WA VIINI LISHE KWENYE CHAKULA
Dalili
  • Kuku hupungua damu, uzito na kudumaa
  • Mifupa huwa laini na kutokuwa imara
  • Hutaga mayai yenye gamba laini na madogo
  • Huwa na manyoya dhaifu
KAZI KWENU WAFUGAJI...!!!!!!